Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Saturday, February 25, 2012

ZOEZI LA AEROBICS LINAVYOSAIDIA KUDHIBITI UZITO WAKO

Mara nyingi tunaongezeka uzito uliokithiri kwa sababu ya kula kupita kiasi virutubisho ambavyo vinatakiwa uwe navyo mwilini mwako na kutumika kwa wakati muafaka.
Hivyo basi ni vema ule vyakula vyenye virutubisho bora na kufanya mazoezi, hii pia hukusaidia mwili wako kupunguza uzito ulokithiri na kuwa na nguvu kwenye misuli yako.

Mazoezi ya Aerobics yanasaidia sana kupunguza mafuta yaliyokithiri kwenye mwili wako kwa wakati muafaka.
Kwamfano ukuwa unafaya mazoezi ya kutembea unaweza kuchoma mpaka kaloriz 210 kwa saa,
halafu ukifanya mazoezi ya mpira wa mikono(hand ball) unachoma kaloriz 600 na unapofanya mazoezi ya Aerobics unachoma kaloriz 700 hadi 860 kwa saa.
Kwa hiyo basi unaona jinsi mazoezi ya Aerobics yalivyo na matokeo mazuri katika kupunguza uzito wa mwili wako, hivyo chaguo ni lako ufanye mazoezi yapi kati ya hayo ambayo nimeyachambua.

















Wadau wa Aerobics wakifaya mazoezi hayo huku
wakifuatilia kwa makini kwa mwalimu wao.

Friday, February 17, 2012

KWA NINI SUKARI NI MUHIMU MWILINI MWAKO

Tukizungumzia sukari ni muhimu kwa binadamu yeyote yule nina maama sukari pia ni uhai au ni moja wapo ya kiungo kinachoupa nguvu misili yako.

Hii ni pamoja nakukupa nguvu na uhai kwenye misuli ya moyo wako.Pamoja na hayo kwa wale wanaofanya mazoezi kila siku ni muhimu kutumia sukari ya kawaida nikuwa na maana kuwa mchujo wa sukari kwenye mwili wake ni wa haraka sana na wa kuaminika kuliko wale wasiofanya mazoezi kabisa.

Sababu ni kwamba anayefanya mazoezi hutokwa na jasho na pia hutumia nguvu katika misuli yake ya mwili hivyo sukari huhitajika mara dufu ya yule asiyefanaya mazoezi ya aina yoyote ile.

Dalili unazosikia kama hauna sukari ya kutosha mwilini hujisikia kuwa na mchoko usioisha kwenye mwili hata kama utajipumzisha kwa siku kadhaa.

Halikadhalika ukiwa unafanya mazoezi utajikuta unakosa nguvu za kuendelea na mazoezi kwa muda mfupi hata wakati huo moyo unakwenda mbio na jasho kukutoka huku ukijisikia vibaya sana na mwili kukosa nguvu.mpaka upate huduma ya kwanza kwa kupatiwa glucose(sukari) ndipo unajisikia vema.

Hii ni tahadhari kwa wale wanaoanza kufanya zoezi la aina yoyote.

Friday, February 10, 2012

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI YA KUJENGA KIFUA KWA KUTUMIA BENCHI PRESS.

Mara nyingi watu ambao hufanya mazoezi, huwa wanatamani kuwa na kifua kilichojengeka na hii ikiwa ni kwa ajili ya kuwa na muonekano mzuri na pindi uvaapo nguo huonekana nadhifu.















Mazoezi ya kujenga kifua wadau wakiwa
wanasimamiana picha ikionyesha namna
ya kuanza zoezi hilo.
















Hapa zoezi la kujenga kifua namna ya kumaliza
ikiwa wamebeba uzito ambao unaumudu.

Monday, February 6, 2012

MAZOEZI YA TUMBO KWA KUTUMIA MPIRA

Katika picha inaonyesha namna ya kuanza zoezi la kupunguza tumbo na namna ya kumlizia
















Katika picha ya kwanza inavyoonyesha jinsi ya
kuanza mazoezi ya kuondoa tumbo unafaya hivyo
kwa kunyanyua mikono yako juu kuvuta pumzi
ndani.















Hapa ni namana ya kumalizia zoezi hilo la tumbo
kwa kutumia mpira.unafanaya hivyo kabadili
mkono na mguu unazungishia chini ya paja lako
mara kwa seti 5x10 halafu unapumziku kwa sekunde
15 na kuanza tena.

















Mdau wa mazoezi ya viungo akifanya mazoezi
ya tumbo picha inaonyesha anavyoanza

















Hapa mazoezi yanavyoishia kwa kupitisha mikono
yako miwili katikati mwa mapaja na mabega ukiwa
umenyanyua unafanya set 3x10

Tuesday, January 31, 2012

FAIDA UNAZOPATA UKIFANYA MAZOEZI MBALIMBALI YA AEROBICS KWA MUDA WA WIKI NNE BILA KUACHA



FAIDA UNAZOPATA KUTOKANA NA MAZOEZI YA AEROBICS

-Kukuongezea uwezo wa kupumua kwa ufasaha na uhakika.

-Kuuweka moyo wako kuwa madhubuti katika msukumo wa damu mwilini.

-Kupunguza mapigo ya moyo ambayo si ya kawaida.

-Kuongeza uwezo wa mzunguko wa damu na kuchuja mafuta kwenye damu kwa

uhakika zaidi.

-Kusaidia kupunguza mafuta kwenye mwili kwa kiasi kikubwa.

-Kusaidia kupunguza uzito ulokithiri.

-Kuongeza mtiririko wa hewa ya oksijeni kwenye damu.

-Kuufanya mwili kuwa na uwezo wa kulainisha misuli ya mwili.

-Kukukinga na maradhi ya mara kwa mara na kuongeza seli nyekundu za mwili.

KWA MASWALI ZAIDI KUHUSU MAZOEZI NIANDIKIE KUPITIA

omaryswai@gmail.com

Thursday, January 26, 2012

WAALIMU WA AEROBICS WAMALIZA KOZI YA AWALI KWA KUFANYA MTIHANI CHUO KIKUU CHA MLIMANI (UDSM PESS)

Katika chuo kikuu cha Mlimani Shule ya Elimu ya Juu,kitengo cha Sayansi mazoezi ya viungo na michezo imemaliza kozi ya awali ya waalimu wa aerobics na gym hivi karibuni kwa kufanya mtihani wa natharia na vitendo.
















Katika picha ya pamoja wanafunzi waliomaliza
kozi ya awali ya aerobics na gym wakiwa na
mwalimu wa aerobics O.Swai aliyevaa kofia
nyekundu.















Hapa ni baadhi ya wanafunzi wakifanya mtihani
wa vitendo wakisimamiwa na mkuu wa kitengo cha
cha PESS Dk. C.Maro ambaye ameshika kitabu
katika picha kati.

Tuesday, January 24, 2012

MAZOEZI YA KICKBOXING KATIKA AEROBICS

Katika mzoezi ya viungo huwa kuna aina nyingi za mazoezi ambayo haya yote hugusa hisia na sehemu mbalimbali za misuli ya mwili wa binaadamu.
Mazoezi hayo ambayo hufanywa kwa kufuata muziki ambao ni maalumu kwa zoezi hilo, yakiwemo mazoezi ya kickbox unafanya kwa kufuatilia muzuki na pindi ufanyapo utasikia kamavile unapigana lakini sivyo ni aina ya mazoezi ya viungo, na pindi umalizapo unasikia akili na mwili wako kweli umefanya zoezi tosha.



















Katika picha hapo juu mwalimu Swai akifundisha
mazoezi ya kickbox ambayo yamependwa sana
na wadau wa aerobics


















Master class Omar swai akiuonyesha mdau wa
aerobics namna ya kutupa ngumi na teke kwa
pamoja.

Wednesday, January 11, 2012

UMUHIMU WA MAZOEZI YA TUMBO

Mara nyingi watu watu huona mazoezi ya tumbo huwa ni magumu sana kwa mtu anayefanya, lakini yana umuhimu wake mkubwa katika maisha ya kila siku.

Umuhimu wa kufanya mazoezi ya tumbo iwe kwa mwanamke au mwanaume unatakikana hii ni kwa ajili ya kuuweka mwili wako katika hali ya kupendeza pindi ukiwa umevaa nguo zako kuweza kukuenea na kuonekana nadhifu na kupendeza.
Hivyo mazoezi ya tumbo pia hukufanya kukazika kwa misuli ya tumbo na kuwa unatembea umenyooka na kuvutia.
















Hapa mwalmu henry akiwa anafanya mazoezi
ya tumbo kwa staili mbali mbali.

Tuesday, January 3, 2012

MAZOEZI YA KUONDOA TUMBO

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI YA TUMBO

Katika picha (a)1 inaonyesha namna ya kuanza kufanya mazoezi ya tumbo na maelezo yake.
Unalala chali kuhakikisha mgongo wako umekandamiza chini kabisa na mikono yako yote miwili ikiwa nyuma ya shingo yako na viwiko vyako vikiwa umenyoosha pande zote, halafu unavuta pumzi ndani kwa kutumia pua kabla ya kunyanyuka


Picha(a)1















Katika picha (b)1 unanyanyuka juu kwa
kunyanyua sehemu ya mabega yako yote
wakati huo unahakikisha unakaza misuli
yatumbo lako pindi unapokuja juu na hapo
ndipo unatoa pumzi kwa kupitia mdomoni
mwako ukiwa una fikia juu na kurudi chini
tena nakuanza kama picha (a)1 invyoonyesha
mara kumi .
unafanya seti 5x10

Picha (b)1






















Zoezi la pili la tumbo picha (a)2 inaonyesha
namna ya kuanza hilo zoezi.
Unakunja muguu yako yote miwili huku
umeweka mikono yako nyuma kwa ajili
ya kujizuia usende nyuma zaidi na kubalasi
mwili wako wakati wa zoezi lenyewe.


Picha(a)2


















Halafu unanyoosha miguu yako kabla ya kufikia kunyooka
unarudia tena kukunja kama picha (a)2 inavyoonyesha.
Kwa kufanya hivyo unatakiwa ufanye mara kumi seti tano
5x10 baada ya hapo unapumzika kwa dakika moja na kurudi
tena.
Usisahau kuvuta pumzi ndani pindi ukunjuapo na kupumua nje
unyooshapo miguu yako.


Picha (b)2



































Friday, December 23, 2011

HERI YA KRISMAS NA MWAKA MPYA WADAU WA MAZOEZI YA VIUNGO POPOTE PALE MLIPO ULIMWENGUNI.

NAWATAKIA KILA LA KHERI KATIKA SIKUKUU YA KRISMASI HII NA MWAKA MPYA KWA WAPENZI WANGU WOTE WA MAZOEZI YA VIUNGO YA AEROBICS POPOTE PALE MLIPO KATIKA ULUMWENGU WA MAZOEZI.

Wakati huu wa sikukuu mara nyingi watu hujiachia na kula bila kuzingatia wanakula nini hii ni kawaida lakini chunga unachokula naufurahishe moyo wako.

Wednesday, December 14, 2011

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA UDSM PESS WANAPOFAIDIKA NA KOZI YA AEROBICS

Katika kozi ya Aerobics sasa inapata umashuhuri mkubwa katika Chuo Kikuu cha Mlimani UDSM katika kitengo cha Elimu ya Sayansi ya michezo.
Hii ikiwa ni kozi ya tatu tangu chuo kikuu cha mlimani kilipoanza kufundisha rasmi,imeonekana kila mwaka wanafunzi wanaongezeka tu hii ni kwa sababu ni kozi ambayo waalimu wa aerobics wanahitajika na mtu hukosi ajira ya ufundishaji iwe kwenye gym za watu binafsi au uwe umejiajiri mwenyewe.


















Katika picha anaonekana mwalimu mwanafunzi
Lulu akiongoza darasa la h/l aerobics PESS DSM.

















Mwalimu mwanafunzi Janifa akiongoza
mazoezi ya step wanafunzi wenzake
UDSM PESS

















Mwalimu wa waalimu Omar Swai (menye kofia
nyekundu)
akiwa katika pozi ya picha na wanafunzi wanao-
somea kozi ya aerobicsPess Udsm.

Thursday, December 1, 2011

NI AINA GANI YA MAJI NA UMUHIMU WA KUNYWA KWA ANAYEFANYA MAZOEZI

Mara nyingi tunapofanya fanya mazoezi iwe ni mazoezi ya viungo au unapocheza mpira na hata unafanya mazoezi ya aina yoyote ile, jua unapunguza maji mwilini mwako kwa kutokwa na jasho unahitaji uongeze maji mwilini mwako.

Lakini kuna watu wengi walipata mafundisho ya kupotoshwa eti huruhusiwi kunywa maji wakati unapofanya mazoezi hadi umemaliza mazoezi na hata ikiwa ni muda wa saa moja au saa mbili hiyo siyo sahihi kabisa.

Mara nyingi unapofanya mazoezi kwanza mwili hupanda joto zaidi ya kawaida, hivyo unahitaji kupoozwa kwa kunywa maji na maji yenyewe yasiwe ya moto kama wengine wanavyojua.
Yawe ni maji ambayo yamepoa yaani yawe na ubaridi kiasi hii husaidia pindi maji yakifika tumboni kuzama mwilini kwa urahisi na kupooza mwili kwa kuteremsha joto lililozidi mwilini.

Pia isiwe baada ya mazoezi bali iwe hata wakati wa mazoezi lakini unywe kiasi cha fundo mbili au tatu kuepuka kichomi.

Kumbuka mwili wako unahitaji maji ya kutosha kwani pasenti 60% ya mwili wako inahitaji maji.
Kunywa maji zaidi ya glasi nane kwa siku.
















Wadau wakifanya mazoezi ya cardio na jasho
huwatoka pia.
















Mazoezi ya Aerobic hutoa jasho sana hivyo maji
ni muhimu wakati wa zoezi na baada ya zoezi.

Thursday, November 17, 2011

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI YA TUMBO KWA KUTUMIA MPIRA MAALUM.

Kwa kawida mazoezi ya kupunguza tumbo yako ya aina mbalimbali na staili nyingi hii yote ni kumsaidia mlengwa mwenye matatizo na kupungua kama sio kuondoka kabisa.
Mazoezi ya tumbo ni ya kufanya kwa muda mrefu na sio kwa msimu tu hivyo inatkiwa kuwa na mazoea ya kufanya mazoezi hayo mara kwa mara.
















Namna ya kuanza zoezi la tumbo kwa kutumia
mpira maalum wa zoezi hilo.
unafanya hilo zoezi mara 25x4 halafu unapumzika
kila baada ya seti moja yaani mara 25. kama picha
inaonyesha juu unavyoanza















Picha ya chini inaonyesha namna ya kumalizia
hilo zoezi la tumbo kwa kutumia mpira maalum

Monday, November 7, 2011

MAZOEZI YA KUJENGA MGONGO KWA KUTUMIA MASHINE

Mazoezi mengi siku hizi yameboreshwa kwa kufanya kwa kutumia mashine kwa uhakika na bila ya kuumia sehemu nyingine ambayo haitakiwi kwa wakati muafaka wa mazoezi.
Kama picha zetu zikionyesha wadau wakifanya mazoezi ya kujenga mgongo.





















Katika picha ya juu inaonyesha namna
ya kuanza zoezi la kujenga mgongo hapo
ni mwana mazoezi Wolter akifanya zoezi.





















Hapa Wolter akimalizia zoezi la kujenga
mgongo huku patna wake wa mazoezi
Maiko akisubiria zamu lake

Thursday, October 27, 2011

NAMNA YA KUTUMIA MASHINE KWA MAZOEZI YA MGONGO

Huwa ni mazoea ya wadau wengi hufikiria mazoezi ya kutumia mashine ni kwa ajili ya wanaume tu hapana.
Mwanamke pia anahitaji kufanya mazoezi kwa kutumia mashine hii humsaidia kupunguza mafuta na kujenga misuli haswa sehemu ya mgongo yaani husaidia kuondoa matairi au manyama uzembe.















Hapa mdau wa mazoezi akifanya mazoezi ya
mgongo akiwa anaazia kama picha inavyoonyesha















Mdauwa mazoezi ya viungo akimalizia kuvuta
kama picha inavyoonyesha akiatimia mashine
nayoitwa rowing.

Tuesday, October 25, 2011

MAZOEZI YA AEROBICS KATIKA CHUO KIKUU CHA MLIMANI DAR ES SALAAM















Wadau wakiwa katika muvment ya mazoezi















Wadau wa mazoezi wa chuo kikuu wakiwa
na mwamko wa mazoezi kwa ajili ya afya
zao. wakiongozwa na mwalimu Swai






























Baadhi ya mazoezi wakifuatilia kwa makini
wadau wa mazoezi udsm mlimani

Sunday, October 16, 2011

KATIKA KUSHEREHEKEA MIAKA HAMSINI YA CHUO KIKUU NA BONANZA LA MAZOEZI YA AEROBICS.

KATIKA KUSHEREHEKEA MIAKA MIAKA HAMSINI YA CHUO KIKUU CHA MLIMANI WANAMICHEZO WOTE WALISHIRIKI KATIKA KUPASHA MISULI KWA MAZOEZI YA AEROBICS YA KIONGOZWA NA MWALIMU OMAR SWAI.















Washiriki wa bonanza wakianza na mazoezi ya
aerobics.
















Ilikuwa ni mambo ya cooldown hapa baada ya
aerobics.
















Mazoezi ya kunyoosha misuli kwa matayarisho
ya wanamichezo wa bonanza hilo lililofanyika
katika viwanja vya Chuo kikuu Mlimani.

Saturday, October 15, 2011

SIKU YA BONANZA CHUO KIKUU CHA DAR ESALAAM MLIMANI NA MIAKA HAMSINI

Katika kusherehekea miaka hamsini ya tangu kuanzishwa kwa chuo kikuu cha Dar es salaamMlimani enzi hizo mpaka hadi leo kulikuwa na sherehe mbali mbali za kushiriki kwenye michezo.



















Hapa akinamama wakijitayarisha kukimbia
mita mia moja siku ya bonanza jumamosi
kwenye viwanja vya chuo kikuu.
















Mbio zilianza hivyo kama inavyookana
hapo juu kwa akina mama.















Akina baba nao walikuwemo katika mashindano
hayo ya mita mia moja.

Friday, October 7, 2011

MIAKA HAMSINI YA CHUO KIKUU DAR ES SALAAM CHA MLIMANI YAFANA KWA MAZOEZI YA VIUNGO.

Katika shamra shamra za kusherehekea miaka hamsini ya Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Mlimani mkuu wa chuo hicho Profesa Mkandala akifungua Gym ya mazoezi ya viungo akiwa anasindikizwa na mkuu wa shule kuu ya elimu Eustella Bhalalusesa ambaye pia kitengo hiko kiko chini yake.





















Profesa Ruwekeza Mkandala akikata utepe rasmi kufungua gym.
















Baada ya kukata utepe Profesa Mkandala alijiunga na mazoezi ya aerobic
pamoja na wadauwengine.















Ilikuwa ni siku ya mazoezi tu wadau wakifurahia
mazoezi ya viungo

Wednesday, September 28, 2011

UMUHIMU WA MATAYARISHO KABLA YA KUANZA MAZOEZI (WARM UP)

Wadau wa mazoezi ya viungo leo ngoja niwakumbushe umuhimu wa kufanya mazoezi ya kupasha mwili moto(warm up) kabla ya kuanza zoezi lolote.

Umuhimu wa kufanya hilo zoezi la kupasha mwili moto(WARM UP) ni kuutayarisha mwili kwa mazoezi. Pia husaidia kuongeza usambazaji wa damu katika viungo pamoja na misuli ya mwili pamoja na kuupa mwii joto kwa matayarisho ya mazoezi utakayofanya ambayo husaidia kulainisha viungo vyako vya mwili, hata hivyo husaidia kulainisha mishipa inayopeleka damu kwenye moyo na kusaidia kulinda misuli isipate madhara pamoja na mifupa.

Vilevile kupasha mwili moto(warm up) husaidia kuongezeka upatikainaji wa hewa ya oksijen kwenye misuli na mishipa ya fahamu kwa binaadamu anayefanya mazoezi.

Hivyo mdaua wa mazoezi huo ndio umuhimu wa kupasha mwili moto( warm up) kabla ya kufanya mazoezi.