Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Friday, February 22, 2013

NAMNA YA KULA MLO WAKATI UNAPOTAKA KUPUNGUA UZITO ULIOZIDI NA MAZOEZI


Kupunguza uzito ulokithiri huchukua muda mpaka kupata matokeo yake,ukiwa unazingatia kufanya mazoezi kama vile kutembea, kuendesha baiskeli na kufanya mazoezi ya aerobics ambayo hukupa matokeo haraka zaidi kuliko mazoezi yoyote yale.

Nikizungumzia mazoezi ya aerobics huwa nina maana kila sehemu ya kiungo cha mwili wako hufanyishwa mazoezi.
Ukizingatia kuanzia mwanzo wa zoezi hilo unaanza na kupasha mwili moto halafu ndio unaendelea na mazoezi mengine huku ukifuatilia ikienda  sambamba na   muziki maalumu kwa mazoezi  tofauti.
Hii hukupa wewe mwanamazoezi kufanya  na kufurahia,baada ya hapo ikifuatiwa na mazoezi kuunnyoosha mwili na kuondoa uchovu kwa kipindi  chote cha mazoezi.
Na kumalizia na zoezi la kuondoa tumbo.

Lakini mazoezi  yanatakiwa uende sambamba na kupunguza chakula kwa mfano ulikuwa unakula sahani iliyojaa unakula nusu yake. Hata hivyo uwe umepata kifungua kinywa cha kutosha itakisaidia kutokula hovyo hovyo.Mchana  utakula kiasi tu  ukipata matunda kwa wingi.
Wakati wa usiku ujitahidi upate chakula chepesi kwani maranyingi chakula cha jioni huongeza uzito kwa sababu ukishakula unaenda kulala na msago wa chakula huwa umesimama hadi kesho yake saa 12 asubuhi.
Pia jitahidi kupunguza mafuta kwenye  chakula hata sukari iwe kiasi na chumvi pia itakusaidia kupunguza uzito.








                     Aina ya mazoezi  ambayo unatakiwa kufanya kama picha  inavyoonyesha

                                 







          Kuna aina nyingi ya mazoezi ambayo husaidia kukupunguza kwa kutumia mashine
                       






















Thursday, February 7, 2013

AINA MBALI MBALI YA MAZEOZI YA VIUNGO(AEROBICS)




Katika kufanya mazoezi ya viungo unaweza pia kufanya mazoezi  kwa kucheza utakavyo ili mradi unaendana na midundo.
Hivi sasa waalimu wa mazoezi haya ya viungo wamegundua namna ya kuwavutia wadau wa mazoezi haya kwa kuwapa mtindo na aina ya muziki







                                             Hapa ni namna  ya kuanza zoezi la kick box






                                         Namna ya kutupa ngumi pamoja kufuatilia mdundo






                                     Jinsi  ya kutumia mateke au kutumia goti uku ukienda na muziki









Mwalimu  Swai akitoa mafunzo namnkukunja na kutupa ngumi