Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Tuesday, April 30, 2013

GYM YA CHUO KIKUU MLIMANI (UDSM) PESS YAFANA KATIKA MAZOEZI YA AEROBICS

Gym maarufu ambayo inaongoza kwa kutoa mafunzo ya waalimu wa aerobics hapa Tanzania na ambayo ina mwalimu aliyebobea katika mazoezi haya hapa Tanzania mwalimu O.Swai inafana kila kukicha kwenye mazoezi haya.Hivyo akitoa wito kwa wanamazoezi kujiunga katika gym hiyo iliyopo chuo kikuu na kupata mazoezi yaliyokwenda shule kama usemi wetu usemavyo Elimu Kwanza.






                              Mwalimu O.Swai akiwa kwenye darasa lake la step aerobics
                                 chuo kikuu cha mlimani




                              Wadau  wa aeobics wakifuatilia bila kukosea mazoezi ya step






                                  Likiwa ni darasa lililoja wadau wa mataifa mbali mbali
                                  wakifuatilia kwa makini mazoezi.






                         Kushoto mwanzo ni mdau wa mazoezi Isabellah akifuatilia kwa makini






                            Mwalimu Swai akiwa kwenye mwendo mdundo katika mazoezi.

Wednesday, April 24, 2013

CLUB YA MAZOEZI YA AEROBICS YA VETA (DSMRVTSC) SASA YAVUMA



 Ni kwa nadra sana kusikia wafanyakazi  kuamua kufanya mazoezi na kwa moyo kama club ya VETA ambayo inavuma kwa sasa kwa ajili ya kufanya mazoezi, hii ni kwa sababu hata viongozi wao wanapenda mazoezi na kuwathamini wafanya kazi wenzao.
Klabu hii hufanya mazoezi mara tatu kwa wiki yaani Jumatatu,Jumatano na Ijumaa wakifundishwa na mwalimu  O.Swai akishirikiana na msaidizi wake mwalimu Sukamba.






                                  Mwalimu Sukamba akiwa kwenye darasa lake la aerobics.


                                 Wanawake wafanyakazi wa veta pia wanashiriki ipasavyo



                              Wafanyakazi wa veta wakiwa na kiongozi wao baser wa chiuo
                                  aliyevaa tishet  njano msitari wa kwanza.




                              Wafanyakazi wengi hufurahia mazoezi  na kupata matokeo
                                 mazuri na kuwa na afya njema.

Tuesday, April 23, 2013

MWALIMU WA AEROBICS ABDALA HERRI ANAVYOWIKA ABUDHABI KATIKA KUTOA AINA MBALI MBALI YA MAZOEZI YA VIUNGO



Mwalimu Abdala Herri ni kijana aliyebobea  sana katika mazoezi haya ya aerobics, hata katika mazoezi ya spin yaani kuendesha darasa la  baskeli maalum kwa mazoezi ya mwili yaitwayo spin bike.
Siyo hayo tu pia huendesha darasa la NRG ambalo unatumia barbell na uzito kwa ajili ya kuondoa manyama uzembe.
Pia hutoa ushauri kwa wateja wake ambao wana matatizo mbali mbali ya afya zao.
Hivi sasa  Abdala yukoAbudhabi akifundisha kwenye Gym ya jeshi la  huko na anatarajia kufungua gym hapa Tanzania na huko Mombasa Kenya.




Mwalimu Abdala yuko mbele  kavaa tisheti nyekundu akiwa anafundisha darasa la spin





                    Hili ni darasa la NRG ambalo Abdala anafanyisha mazoezi yake ya mapaja.
                     (squat)kwa ajili ya kujenga misuli wa mbele ya paja





Abdala Herri akionyesha mazoezi kwa ajili ya kujenga misuli ya mgongo





                           Zoezi likiwa limepamba moto yakiongozwa na mwalimu Abdala. Herri.


Friday, April 12, 2013

KOZI YA AEROBICS INAYOFANYIKA CHUO KIKUU MLIMANI YAFANA SANA MWAKA HUU 2013


Katika kitengo cha Physical Education and Sport Science(PESS) Ambayo iko chini ya Shule Kuu ya Elimu hapa  Chuo Kikuu Mlimani(School of  Educatio) hutoa mafunzo maalum ya aina yote ya michezo kwa waalimu ikiwemo mafunzo ya mpira wa miguu, kuogelea,long tenise, basketball handball netball, badminto, mpira wa meza(table tenis), riadha, american foot ball  na pia hutoa mafunzo ya Aerobics kwa waalimu wa mazoezi ya viungo.

Kozi ya Aerobics mwaka huu imependwa sana na kushiriki wanafunzi wengi zaidi wakiwemo wa hapa nchini Tanzania, China na nchi za Scandnavia pia wameshiriki kozi hii ambayo itawasaidia katika maisha yao ya baadae pindi wamalizapo chuo kwa kupata ajira au kufundisha mashuleni.

Kwenye kozi hii akiongozwa na mkuu wa kitengo cha Michezo na Sayansi Dr.S. Maro akisaidiana na Mwalimu  wa Fitness O.Swai kimekwisha toa mafunzo  kwa wanafunzi wasiopungua 70 ambao walimaliza hapa mafunzo yao ikiwa  ni pamoja na Aerobics and Fitness.





              Mwalimu Swai akiwa na wanafunzi wake kutoka  China ambao wako na furaha.

 


                 Mwalimu mwanafunzi akijaribu kutoa mazoezi aliyofundishwa katika hio somo.




                         Mwanafunzi Safia kutoka China akiongoza darasa mazoezi ya Aerobics.



       Hapa Safia akionyesha ujasiri wa kufundisha darasa la mazoezi ya viungo (aerobics)




  Hili ni darasa mchanganyiko wa wanataaluma wa mazoezi ya viungo wakifuatilia kwa makini.





Kila mwanafunzi  hufurahia wanavyopata mavunzo kutoka kwa mwalimu O.Swai na kumuelewa vema









Thursday, March 14, 2013

MAZOEZI YA AEROBICS YAFANA MJINI MOROGORO






Wakazi wa Morogoro mji uliozungukwa na milima ya uluguru na hali ya hewa nzuri,wakiwa na hamasa kubwa kufanya mazoezi ya viungo kwa afya yao, huku wakiongozwa na mwalimu Musiba  Manyama ambaye ni mwalimu wa siku nyingi katika fani hii.
Gym hii ya mazoezi inaitwa SIMBA OIL GYM iliyopo katika majengo hayo ya Simba oil kituo cha petroli cha mjini Morogoro.


                       Mwalimu Musiba akiwa  katikati  ya wanafunzi akitoa mazoezi ya
                          kunyoosha viungo baada ya zoezi kuisha.




                          Hapa ni mwalimu  mwalikwa   Payas (mwenye kofia) kutoka Dar
                          ambaye ni mkurugenzi wa gym ya Fitness for Life akitoa mazoezi




                                      Kina dada wa Moro nao hawapo nyuma kwa kufanya
                                        mazoezi kwa afya zao




                                  Mwalimu musiba akifanya mazoezi na wadau wake wa
                                       Morogoro .Simba Oili Gym

Friday, February 22, 2013

NAMNA YA KULA MLO WAKATI UNAPOTAKA KUPUNGUA UZITO ULIOZIDI NA MAZOEZI


Kupunguza uzito ulokithiri huchukua muda mpaka kupata matokeo yake,ukiwa unazingatia kufanya mazoezi kama vile kutembea, kuendesha baiskeli na kufanya mazoezi ya aerobics ambayo hukupa matokeo haraka zaidi kuliko mazoezi yoyote yale.

Nikizungumzia mazoezi ya aerobics huwa nina maana kila sehemu ya kiungo cha mwili wako hufanyishwa mazoezi.
Ukizingatia kuanzia mwanzo wa zoezi hilo unaanza na kupasha mwili moto halafu ndio unaendelea na mazoezi mengine huku ukifuatilia ikienda  sambamba na   muziki maalumu kwa mazoezi  tofauti.
Hii hukupa wewe mwanamazoezi kufanya  na kufurahia,baada ya hapo ikifuatiwa na mazoezi kuunnyoosha mwili na kuondoa uchovu kwa kipindi  chote cha mazoezi.
Na kumalizia na zoezi la kuondoa tumbo.

Lakini mazoezi  yanatakiwa uende sambamba na kupunguza chakula kwa mfano ulikuwa unakula sahani iliyojaa unakula nusu yake. Hata hivyo uwe umepata kifungua kinywa cha kutosha itakisaidia kutokula hovyo hovyo.Mchana  utakula kiasi tu  ukipata matunda kwa wingi.
Wakati wa usiku ujitahidi upate chakula chepesi kwani maranyingi chakula cha jioni huongeza uzito kwa sababu ukishakula unaenda kulala na msago wa chakula huwa umesimama hadi kesho yake saa 12 asubuhi.
Pia jitahidi kupunguza mafuta kwenye  chakula hata sukari iwe kiasi na chumvi pia itakusaidia kupunguza uzito.








                     Aina ya mazoezi  ambayo unatakiwa kufanya kama picha  inavyoonyesha

                                 







          Kuna aina nyingi ya mazoezi ambayo husaidia kukupunguza kwa kutumia mashine
                       






















Thursday, February 7, 2013

AINA MBALI MBALI YA MAZEOZI YA VIUNGO(AEROBICS)




Katika kufanya mazoezi ya viungo unaweza pia kufanya mazoezi  kwa kucheza utakavyo ili mradi unaendana na midundo.
Hivi sasa waalimu wa mazoezi haya ya viungo wamegundua namna ya kuwavutia wadau wa mazoezi haya kwa kuwapa mtindo na aina ya muziki







                                             Hapa ni namna  ya kuanza zoezi la kick box






                                         Namna ya kutupa ngumi pamoja kufuatilia mdundo






                                     Jinsi  ya kutumia mateke au kutumia goti uku ukienda na muziki









Mwalimu  Swai akitoa mafunzo namnkukunja na kutupa ngumi



Monday, January 21, 2013

MBAGALA JOGGING CLUB WAKARIBISHWA VETA CLUB KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA

                                             
Klabu ya mazoezi ya viungo ya  VETA    chuo cha ufundi stadi  Dar es salaam ikiwa imewakaribisha wanamazoezi wenzao kutoka klabu ya Mbagala Joging ikiongozwa na mwalimu wao Adam Gwao ambaye pia ni muasisi wa club hiyo. Mazoezi hayo yalifana sana ambayo yalianza  majira ya  saa 12 hadi saa moja asubuhi  yakiwa yamehudhuriwa na wakuu wa chuo hicho cha  Veta.
                                                                                                                        











    Mwalimu Swai  akikakaribisha wanamazoezi  wenzake kutoka  Mbagala  Jogging  club
    akiwa mbele ya wanamazoezi na mwalimu  Adam Gwao tayari kuanza zoezi la Aerobics

                                                                               

                                                                                           



   Mazoezi yameanza pamoja na mkuu wa chuo cha Veta (mwenye fulana ya bluu ) akiwa
   mstari wa mbele.
                     





               Zoezi lilipamba moto kila mtu akiwa  mwenye furaha  asubuhi hiyo ya mazoezi





        Kila mtu alikuwa na usongo wa kufanya zoezi siku hiyo bila kushindwa au kuchoka







               Mkuu  wa chuo cha Veta  Mr. Samwel Ng'andu  akizungumza na wanamazoezi
              na kuwakaribisha wanamazoezi wa Mbagala club  wote wakimsikiliza kwa makini.



                                                                               



     Mwalimu O.Swai akitoa mafunzo ya lishe bora baada ya kumaliza mazoezi ya siku hiyo
     Akisema "Kufanya mazoezi peke yake hayasaidi ila ni pamoja na kujaribu kubadili tabia
       ya  kula mlo".



















































Friday, January 4, 2013

WAFANYAKAZI WA VETA WAITIKIA WITO WA KUFANYA MAZOEZI KWA AFYA ZAO.



Kwa kaweli ni jambo la kutia moyo kwa wafanyakazi wa VETA kuanzisha club yao ya mazoezi

japo mara moja kwa wiki  ambapo hukutana na kufanya joging  wakimalizia na mazoezi ya viungo.

Mwaka  huu wa 2013 wamepania zaidi kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zao bili kujali nyadhifa zao.








                             Hapa ni  pamoja na mkuu  wa chuo  hicho akiwa mastari wa mbele.






                             Wafanyakazi  wa veta wakiwa  wanafurahia mazoezi  hapo chuoni

                   










Monday, December 24, 2012

HERI YA MWAKA MPYA 2013 WANAMAZOEZI


                        Mazoezi ya kupunguza mafuta kwenye tumbo

OK  BODY SHAPE     INAWATAKIA  HERI  YA 

***************************************************** 

MWAKA MPYA    2013

******************************************************


NAWATAKIA  MAFANIKIO MEMA  KATIKA  MAISHA YA KILA SIKU


NA KUKARIBISHA  MWAKA MPYA WA  2013  KWA FURAHA NA 

SHANGWE.



****************************************************                   




               --MAZOEZI NI MAISHA YA KILA SIKU--

                   +++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

     

               FANYA MAZOEZI KWA  AFYA BORA NA KUREFUSHA UMRI WAKO

   ******************************************************

Thursday, December 13, 2012

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI YA KUJENGA MABEGA (SHOULDER PRESS)

Picha ya kwanza inaonyesha namna ya kuanza zoezi hilo la shoulder


                                 Hatua ya pili unavyonyanyua uzito kwa kujenga misuli ya mabega
                         



 Hapa  ndipo unapofika  hatua ya mwisho ya kunyanyua uzito huku umeketi.





Mazoezi haya mara nyingi huwa ni magumu na yenye maumivu pindi umalizapo au wakati unapofanya ,hata wakati mwingine unaweza kukata tamaa kuyafanya lakini mtu ukitaka kujenga hiyo misuli uwe na moyo wakufanya na kurudia huku ukiongeza uzito.Pia uwe unafanya seti nyingi zaidi hii itakusaidia kujenga misuli yako na kukua kwa haraka zaidi.yaani unafanya seti tatu mara 12-15 kwa kuanza na uzito mdogo halafu unaongeza kwenye seti ya tano na ya sita kwa kufanya mara 6-8 halafu unaongeza tena uzito na kufanya mara 4 kwa seti mbili. Kwa maelekezo haya utaweza kujenga shoulder zako upendavyo.





































Thursday, November 29, 2012

FAIDA YA KUFANYA MAZOEZI YA AEROBICS KWA WALE WENYE KIFUA CHA PUMU.

Leo nimeona umuhimu wa kuzungumzia kuhusu wale ambao wanasumbuliwa na ugonjwa wa kifua cha pumu.
Mazoezi ni muhimu sana haswa  kwa wale ambao wanasumbuliwa na kifua cha pumu, hii nimesemea kwa sababu kuna watu ambao husumbuliwa na pumu muda mrefu maana wengine huzaliwa nayo hata pia kwa wale wnaosumbuliwa na maradhi ya kisukari mazoezi  huwasaidia sana katika kuugua mara kwa mara.
Kwa uthibitisho wa utafiti wangu nimeona wengi waliofanya mazoezi hupata nafuu ya hali ya juu na kupunguza matumizi ya dawa za pumu kwa sababu mazoezi humsaidia kumuwezesha kupumua na kufanaya mapafu yake kufanaya kazi ipasavyo. Hivyo nawashauri wale wenye matatizo haya kujiunga  na club za mazoezi na kufanya mazoezi ya Aerobics yatasaidia kama kupunguza na kutibika kabisa.


                     Mazoezi  ya kutembea  au kukimbia kwa kutumia mashine ya treadmill


                  Mazoezi ya aerobics ambayo pia ni njia muhimu katika kukusaidia kupunguza
                       na kutibu ugonjwa wa kifua cha pumu.

Tuesday, November 20, 2012

WAFANYA KAZI WA VETA(DSMRVTSC) WAFUNGUA CLUB YA MAZOEZI HAPO VETA KWA WAFANYAKAZI WOTE.


 Katika mazungumzo na wakuu wa hapo DSMRVTSC VETA walisema wameamua kuanzisha club yao ya mazoezi hii ni kutokana na kutokuwa na muda wa kufanya mazoezi siku za wiki na kuamua kufanya mazoezi angalau siku ya Jumamosi na jumapili hapo baadae.Kwa sasa wanafanya mazoezi kila Jumamosi asubuhi kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa moja.






Wanamazoezi wa  Veta wakifanya mazoezi ya viungo kwenye  gym yao wakiwa na mwalimu  O.Swai



Hapa ni mkuu wa chuo hicho Samwel Ng'andu  akiongoza wafanyakazi wenzake katika  zoezi kila asubuhi ya Jumamosi alifungua rasmi.



                                      Mazoezi yakiwa yamepamba moto katika club hiyo Veta


                                 Mwalimu Swai akirekebisha wana mazoezi na kuwapa moyo












Friday, November 16, 2012

MAZOEZI YA KUJENGA MAPAJA KWA KUTUMIA BARBELL(free weight)

                                                                                                     

Mara nyingi wanamazoezi wa kujenga misuli husahau kufanya mazoezi ya kujenga misuli ya miguu, hii ni tatizo haswa kwa wale ambao wanaanza zoezi hili la kujenga misuli.
Nikisema hivyo nina maana wao huanza kujenga sehemu ya mikono na kifua ikiwa sehemu hiyo inaonekana aidha kwa kuvaa tisheti lakini  hii ikiwa ni staili ya vijana.
Kumbuka mazoezi ya miguu ni uhimu sana kwa wale wanaofanya mazoezi ya kujenga misuli ili uonekane nadhifu zaidi





                                           Hapa katika picha inaonyesha  kijana Jonathan
                                              akianza zoezi la kujenga miguu kwenye gym ya
                                                Chuo  Kikuu cha Mlimani UDSM.





                                            Hapa Jonathan akimaliza zoezi hilo kwa hesabu
                                               ya 10x4 na kuongeza uzito kila seti. 


Wednesday, November 7, 2012

MAZOEZI YA KUJENGA SEHEMU YA MSULI WA NYUMA WA MKONO(TRICEPS)


Ukiwa unafanya mazoezi ya triceps kwa kutumia cable mashine mara nyingi huwa ni mazoezi ambayo yana matokeo mazuri na uhakika.
Mazoezi haya unafanya kwa marudio ya seti 4 x 12 na unapoongeza uzito ndipo unapo punguza hesabu ya kufanya.





                                    Mwalimu wa mazoezi  akionyesha  namna ya kuanza zoezi hilo




                                    Mwalimu Swai akionyesha jinsi ya kumalizia zoezi la triceps