Gym maarufu ambayo inaongoza kwa kutoa mafunzo ya waalimu wa aerobics hapa Tanzania na ambayo ina mwalimu aliyebobea katika mazoezi haya hapa Tanzania mwalimu O.Swai inafana kila kukicha kwenye mazoezi haya.Hivyo akitoa wito kwa wanamazoezi kujiunga katika gym hiyo iliyopo chuo kikuu na kupata mazoezi yaliyokwenda shule kama usemi wetu usemavyo Elimu Kwanza.
Mwalimu O.Swai akiwa kwenye darasa lake la step aerobics
chuo kikuu cha mlimani
Wadau wa aeobics wakifuatilia bila kukosea mazoezi ya step
Likiwa ni darasa lililoja wadau wa mataifa mbali mbali
wakifuatilia kwa makini mazoezi.
Kushoto mwanzo ni mdau wa mazoezi Isabellah akifuatilia kwa makini
Mwalimu Swai akiwa kwenye mwendo mdundo katika mazoezi.
OK BODY SHAPE
Hii ni blog mahususi kwa mazoezi ya viungo ambayo ni muhimu kwa afya zetu
Tuesday, April 30, 2013
Wednesday, April 24, 2013
CLUB YA MAZOEZI YA AEROBICS YA VETA (DSMRVTSC) SASA YAVUMA
Ni kwa nadra sana kusikia wafanyakazi kuamua kufanya mazoezi na kwa moyo kama club ya VETA ambayo inavuma kwa sasa kwa ajili ya kufanya mazoezi, hii ni kwa sababu hata viongozi wao wanapenda mazoezi na kuwathamini wafanya kazi wenzao.
Klabu hii hufanya mazoezi mara tatu kwa wiki yaani Jumatatu,Jumatano na Ijumaa wakifundishwa na mwalimu O.Swai akishirikiana na msaidizi wake mwalimu Sukamba.
Mwalimu Sukamba akiwa kwenye darasa lake la aerobics.
Wanawake wafanyakazi wa veta pia wanashiriki ipasavyo
Wafanyakazi wa veta wakiwa na kiongozi wao baser wa chiuo
aliyevaa tishet njano msitari wa kwanza.
Wafanyakazi wengi hufurahia mazoezi na kupata matokeo
mazuri na kuwa na afya njema.
Tuesday, April 23, 2013
MWALIMU WA AEROBICS ABDALA HERRI ANAVYOWIKA ABUDHABI KATIKA KUTOA AINA MBALI MBALI YA MAZOEZI YA VIUNGO
Mwalimu Abdala Herri ni kijana aliyebobea sana katika mazoezi haya ya aerobics, hata katika mazoezi ya spin yaani kuendesha darasa la baskeli maalum kwa mazoezi ya mwili yaitwayo spin bike.
Siyo hayo tu pia huendesha darasa la NRG ambalo unatumia barbell na uzito kwa ajili ya kuondoa manyama uzembe.
Pia hutoa ushauri kwa wateja wake ambao wana matatizo mbali mbali ya afya zao.
Hivi sasa Abdala yukoAbudhabi akifundisha kwenye Gym ya jeshi la huko na anatarajia kufungua gym hapa Tanzania na huko Mombasa Kenya.
Mwalimu Abdala yuko mbele kavaa tisheti nyekundu akiwa anafundisha darasa la spin
Hili ni darasa la NRG ambalo Abdala anafanyisha mazoezi yake ya mapaja.
(squat)kwa ajili ya kujenga misuli wa mbele ya paja
Abdala Herri akionyesha mazoezi kwa ajili ya kujenga misuli ya mgongo
Zoezi likiwa limepamba moto yakiongozwa na mwalimu Abdala. Herri.
Friday, April 12, 2013
KOZI YA AEROBICS INAYOFANYIKA CHUO KIKUU MLIMANI YAFANA SANA MWAKA HUU 2013
Katika kitengo cha Physical Education and Sport Science(PESS) Ambayo iko chini ya Shule Kuu ya Elimu hapa Chuo Kikuu Mlimani(School of Educatio) hutoa mafunzo maalum ya aina yote ya michezo kwa waalimu ikiwemo mafunzo ya mpira wa miguu, kuogelea,long tenise, basketball handball netball, badminto, mpira wa meza(table tenis), riadha, american foot ball na pia hutoa mafunzo ya Aerobics kwa waalimu wa mazoezi ya viungo.
Kozi ya Aerobics mwaka huu imependwa sana na kushiriki wanafunzi wengi zaidi wakiwemo wa hapa nchini Tanzania, China na nchi za Scandnavia pia wameshiriki kozi hii ambayo itawasaidia katika maisha yao ya baadae pindi wamalizapo chuo kwa kupata ajira au kufundisha mashuleni.
Kwenye kozi hii akiongozwa na mkuu wa kitengo cha Michezo na Sayansi Dr.S. Maro akisaidiana na Mwalimu wa Fitness O.Swai kimekwisha toa mafunzo kwa wanafunzi wasiopungua 70 ambao walimaliza hapa mafunzo yao ikiwa ni pamoja na Aerobics and Fitness.
Mwalimu Swai akiwa na wanafunzi wake kutoka China ambao wako na furaha.
Mwalimu mwanafunzi akijaribu kutoa mazoezi aliyofundishwa katika hio somo.
Mwanafunzi Safia kutoka China akiongoza darasa mazoezi ya Aerobics.
Hapa Safia akionyesha ujasiri wa kufundisha darasa la mazoezi ya viungo (aerobics)
Hili ni darasa mchanganyiko wa wanataaluma wa mazoezi ya viungo wakifuatilia kwa makini.
Kila mwanafunzi hufurahia wanavyopata mavunzo kutoka kwa mwalimu O.Swai na kumuelewa vema
Thursday, March 14, 2013
MAZOEZI YA AEROBICS YAFANA MJINI MOROGORO
Wakazi wa Morogoro mji uliozungukwa na milima ya uluguru na hali ya hewa nzuri,wakiwa na hamasa kubwa kufanya mazoezi ya viungo kwa afya yao, huku wakiongozwa na mwalimu Musiba Manyama ambaye ni mwalimu wa siku nyingi katika fani hii.
Gym hii ya mazoezi inaitwa SIMBA OIL GYM iliyopo katika majengo hayo ya Simba oil kituo cha petroli cha mjini Morogoro.
Mwalimu Musiba akiwa katikati ya wanafunzi akitoa mazoezi ya
kunyoosha viungo baada ya zoezi kuisha.
Hapa ni mwalimu mwalikwa Payas (mwenye kofia) kutoka Dar
ambaye ni mkurugenzi wa gym ya Fitness for Life akitoa mazoezi
Kina dada wa Moro nao hawapo nyuma kwa kufanya
mazoezi kwa afya zao
Mwalimu musiba akifanya mazoezi na wadau wake wa
Morogoro .Simba Oili Gym
Friday, February 22, 2013
NAMNA YA KULA MLO WAKATI UNAPOTAKA KUPUNGUA UZITO ULIOZIDI NA MAZOEZI
Kupunguza uzito ulokithiri huchukua muda mpaka kupata matokeo yake,ukiwa unazingatia kufanya mazoezi kama vile kutembea, kuendesha baiskeli na kufanya mazoezi ya aerobics ambayo hukupa matokeo haraka zaidi kuliko mazoezi yoyote yale.
Nikizungumzia mazoezi ya aerobics huwa nina maana kila sehemu ya kiungo cha mwili wako hufanyishwa mazoezi.
Ukizingatia kuanzia mwanzo wa zoezi hilo unaanza na kupasha mwili moto halafu ndio unaendelea na mazoezi mengine huku ukifuatilia ikienda sambamba na muziki maalumu kwa mazoezi tofauti.
Hii hukupa wewe mwanamazoezi kufanya na kufurahia,baada ya hapo ikifuatiwa na mazoezi kuunnyoosha mwili na kuondoa uchovu kwa kipindi chote cha mazoezi.
Na kumalizia na zoezi la kuondoa tumbo.
Lakini mazoezi yanatakiwa uende sambamba na kupunguza chakula kwa mfano ulikuwa unakula sahani iliyojaa unakula nusu yake. Hata hivyo uwe umepata kifungua kinywa cha kutosha itakisaidia kutokula hovyo hovyo.Mchana utakula kiasi tu ukipata matunda kwa wingi.
Wakati wa usiku ujitahidi upate chakula chepesi kwani maranyingi chakula cha jioni huongeza uzito kwa sababu ukishakula unaenda kulala na msago wa chakula huwa umesimama hadi kesho yake saa 12 asubuhi.
Pia jitahidi kupunguza mafuta kwenye chakula hata sukari iwe kiasi na chumvi pia itakusaidia kupunguza uzito.
Aina ya mazoezi ambayo unatakiwa kufanya kama picha inavyoonyesha
Kuna aina nyingi ya mazoezi ambayo husaidia kukupunguza kwa kutumia mashine
Thursday, February 7, 2013
AINA MBALI MBALI YA MAZEOZI YA VIUNGO(AEROBICS)
Katika kufanya mazoezi ya viungo unaweza pia kufanya mazoezi kwa kucheza utakavyo ili mradi unaendana na midundo.
Hivi sasa waalimu wa mazoezi haya ya viungo wamegundua namna ya kuwavutia wadau wa mazoezi haya kwa kuwapa mtindo na aina ya muziki
Hapa ni namna ya kuanza zoezi la kick box
Namna ya kutupa ngumi pamoja kufuatilia mdundo
Jinsi ya kutumia mateke au kutumia goti uku ukienda na muziki
Mwalimu Swai akitoa mafunzo namnkukunja na kutupa ngumi
Monday, January 21, 2013
MBAGALA JOGGING CLUB WAKARIBISHWA VETA CLUB KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA
Klabu ya mazoezi ya viungo ya VETA chuo cha ufundi stadi Dar es salaam ikiwa imewakaribisha wanamazoezi wenzao kutoka klabu ya Mbagala Joging ikiongozwa na mwalimu wao Adam Gwao ambaye pia ni muasisi wa club hiyo. Mazoezi hayo yalifana sana ambayo yalianza majira ya saa 12 hadi saa moja asubuhi yakiwa yamehudhuriwa na wakuu wa chuo hicho cha Veta.
akiwa mbele ya wanamazoezi na mwalimu Adam Gwao tayari kuanza zoezi la Aerobics
Mazoezi yameanza pamoja na mkuu wa chuo cha Veta (mwenye fulana ya bluu ) akiwa
mstari wa mbele.
Zoezi lilipamba moto kila mtu akiwa mwenye furaha asubuhi hiyo ya mazoezi
Kila mtu alikuwa na usongo wa kufanya zoezi siku hiyo bila kushindwa au kuchoka
Mkuu wa chuo cha Veta Mr. Samwel Ng'andu akizungumza na wanamazoezi
na kuwakaribisha wanamazoezi wa Mbagala club wote wakimsikiliza kwa makini.
Mwalimu O.Swai akitoa mafunzo ya lishe bora baada ya kumaliza mazoezi ya siku hiyo
Akisema "Kufanya mazoezi peke yake hayasaidi ila ni pamoja na kujaribu kubadili tabia
ya kula mlo".
Friday, January 4, 2013
WAFANYAKAZI WA VETA WAITIKIA WITO WA KUFANYA MAZOEZI KWA AFYA ZAO.
Kwa kaweli ni jambo la kutia moyo kwa wafanyakazi wa VETA kuanzisha club yao ya mazoezi
japo mara moja kwa wiki ambapo hukutana na kufanya joging wakimalizia na mazoezi ya viungo.
Mwaka huu wa 2013 wamepania zaidi kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zao bili kujali nyadhifa zao.
Hapa ni pamoja na mkuu wa chuo hicho akiwa mastari wa mbele.
Wafanyakazi wa veta wakiwa wanafurahia mazoezi hapo chuoni
Monday, December 24, 2012
HERI YA MWAKA MPYA 2013 WANAMAZOEZI
Mazoezi ya kupunguza mafuta kwenye tumbo
OK BODY SHAPE INAWATAKIA HERI YA
*****************************************************
MWAKA MPYA 2013
******************************************************
NAWATAKIA MAFANIKIO MEMA KATIKA MAISHA YA KILA SIKU
NA KUKARIBISHA MWAKA MPYA WA 2013 KWA FURAHA NA
SHANGWE.
****************************************************
--MAZOEZI NI MAISHA YA KILA SIKU--
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
FANYA MAZOEZI KWA AFYA BORA NA KUREFUSHA UMRI WAKO
******************************************************
Thursday, December 13, 2012
NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI YA KUJENGA MABEGA (SHOULDER PRESS)
Picha ya kwanza inaonyesha namna ya kuanza zoezi hilo la shoulder
Hatua ya pili unavyonyanyua uzito kwa kujenga misuli ya mabega
Hapa ndipo unapofika hatua ya mwisho ya kunyanyua uzito huku umeketi.
Mazoezi haya mara nyingi huwa ni magumu na yenye maumivu pindi umalizapo au wakati unapofanya ,hata wakati mwingine unaweza kukata tamaa kuyafanya lakini mtu ukitaka kujenga hiyo misuli uwe na moyo wakufanya na kurudia huku ukiongeza uzito.Pia uwe unafanya seti nyingi zaidi hii itakusaidia kujenga misuli yako na kukua kwa haraka zaidi.yaani unafanya seti tatu mara 12-15 kwa kuanza na uzito mdogo halafu unaongeza kwenye seti ya tano na ya sita kwa kufanya mara 6-8 halafu unaongeza tena uzito na kufanya mara 4 kwa seti mbili. Kwa maelekezo haya utaweza kujenga shoulder zako upendavyo.
Thursday, November 29, 2012
FAIDA YA KUFANYA MAZOEZI YA AEROBICS KWA WALE WENYE KIFUA CHA PUMU.
Leo nimeona umuhimu wa kuzungumzia kuhusu wale ambao wanasumbuliwa na ugonjwa wa kifua cha pumu.
Mazoezi ni muhimu sana haswa kwa wale ambao wanasumbuliwa na kifua cha pumu, hii nimesemea kwa sababu kuna watu ambao husumbuliwa na pumu muda mrefu maana wengine huzaliwa nayo hata pia kwa wale wnaosumbuliwa na maradhi ya kisukari mazoezi huwasaidia sana katika kuugua mara kwa mara.
Kwa uthibitisho wa utafiti wangu nimeona wengi waliofanya mazoezi hupata nafuu ya hali ya juu na kupunguza matumizi ya dawa za pumu kwa sababu mazoezi humsaidia kumuwezesha kupumua na kufanaya mapafu yake kufanaya kazi ipasavyo. Hivyo nawashauri wale wenye matatizo haya kujiunga na club za mazoezi na kufanya mazoezi ya Aerobics yatasaidia kama kupunguza na kutibika kabisa.
Mazoezi ya kutembea au kukimbia kwa kutumia mashine ya treadmill
Mazoezi ya aerobics ambayo pia ni njia muhimu katika kukusaidia kupunguza
na kutibu ugonjwa wa kifua cha pumu.
Tuesday, November 20, 2012
WAFANYA KAZI WA VETA(DSMRVTSC) WAFUNGUA CLUB YA MAZOEZI HAPO VETA KWA WAFANYAKAZI WOTE.
Katika mazungumzo na wakuu wa hapo DSMRVTSC VETA walisema wameamua kuanzisha club yao ya mazoezi hii ni kutokana na kutokuwa na muda wa kufanya mazoezi siku za wiki na kuamua kufanya mazoezi angalau siku ya Jumamosi na jumapili hapo baadae.Kwa sasa wanafanya mazoezi kila Jumamosi asubuhi kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa moja.
Wanamazoezi wa Veta wakifanya mazoezi ya viungo kwenye gym yao wakiwa na mwalimu O.Swai
Hapa ni mkuu wa chuo hicho Samwel Ng'andu akiongoza wafanyakazi wenzake katika zoezi kila asubuhi ya Jumamosi alifungua rasmi.
Mazoezi yakiwa yamepamba moto katika club hiyo Veta
Mwalimu Swai akirekebisha wana mazoezi na kuwapa moyo
Friday, November 16, 2012
MAZOEZI YA KUJENGA MAPAJA KWA KUTUMIA BARBELL(free weight)
Mara nyingi wanamazoezi wa kujenga misuli husahau kufanya mazoezi ya kujenga misuli ya miguu, hii ni tatizo haswa kwa wale ambao wanaanza zoezi hili la kujenga misuli.
Nikisema hivyo nina maana wao huanza kujenga sehemu ya mikono na kifua ikiwa sehemu hiyo inaonekana aidha kwa kuvaa tisheti lakini hii ikiwa ni staili ya vijana.
Kumbuka mazoezi ya miguu ni uhimu sana kwa wale wanaofanya mazoezi ya kujenga misuli ili uonekane nadhifu zaidi
Hapa katika picha inaonyesha kijana Jonathan
akianza zoezi la kujenga miguu kwenye gym ya
Chuo Kikuu cha Mlimani UDSM.
Hapa Jonathan akimaliza zoezi hilo kwa hesabu
ya 10x4 na kuongeza uzito kila seti.
Wednesday, November 7, 2012
MAZOEZI YA KUJENGA SEHEMU YA MSULI WA NYUMA WA MKONO(TRICEPS)
Ukiwa unafanya mazoezi ya triceps kwa kutumia cable mashine mara nyingi huwa ni mazoezi ambayo yana matokeo mazuri na uhakika.
Mazoezi haya unafanya kwa marudio ya seti 4 x 12 na unapoongeza uzito ndipo unapo punguza hesabu ya kufanya.
Mwalimu wa mazoezi akionyesha namna ya kuanza zoezi hilo
Mwalimu Swai akionyesha jinsi ya kumalizia zoezi la triceps
Subscribe to:
Posts (Atom)






























