Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Thursday, December 17, 2015

FAIDA YA KUNYOOSHA MWILI (STRETCHING EXERCISE) BAADA YA KUMALIZA MAZOEZI.


Wana mazoezi wengi hawazingatii kufanya mazoezi ya kunyoosha mwili(stretching exercise) baada ya kumaliza zoezi husika ipasavyo.

Kwa kufanya mazoezi ya kunyoosha misuli(stretching exercise) husaidia kwa kiasi kikubwa kukuepusha  maumivu yamisuli mwilini mwa mwana mazoezi na kusaidia kuirudisha misuli yako kwenye hali yake ya kawaida. Nikimaanisha kuwa pindi ufanyapo mazoezi misuli ya mwili huwa mifupi na kukaza kwa ajili ya kukupa uwezo na nguvu kipindi ufanyapo mazoezi, misuli hutanuka ili kukupa nguvu zaidi. Ili irejee katika hali yake ya kawaidi ni muhimu sana kufanya mazoezi ya kunyoosha misuli(stretching) baada ya mazoezi.

Lakini  ukumbuke huwezi nyoosha misuli (stretching) kabla ya kupasha misuli joto(warm up). Hii husaidia kutayarisha misuli yako kwa kuipa joto na kupeleka mapigo ya moyo wako sambamba kwa zoezi lifuatalo, pia kuepuka kuumia kwa misuli wakati wa mazoezi. Kunyoosha mwili (stretching) husaidia kupunguza msongamano wa mawazo.Tafiti zimeonyesha pia husaidia kuondoa ganzi na kuwa mchangamfu wa misuli kwa kufanya mazoezi ya kunyoosha mwili(stretching) kila siku


                  Wanamazoezi ya Aerobics wakinyoosha mwili(stretching) baada ya zoezi


Sunday, November 8, 2015

NAMNA YA KUDHIBITI UZITO BAADA YA KUFIKIA MALENGO YA KUPUNGUZA UZITO ULOKITHIRI


Mara nyingi  mwana mazoezi hujisahau pindi akifikia lengo lake la kupungua uzito katika kudhibiti chakula anachokula.

Katika kusema hivyo ni pamoja na kuepuka kula mafuta kwa kiwango kikubwa, kuepuka kula vyakula  bila kuzingatia muda wa kupata mlo.

Jambo la muhimu ni kukumbuka kula chakula chepesi nyakati za usiku kwa kuepuka kuongezeka uzito  kunywa maji ya kutosha na kupata muda wa kulala usiopungua masaa nane. 

Tuesday, October 6, 2015

AINA ZA MAZOEZI YA TUMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA UKIWA SEHEMU YOYOTE


Mara nyingi mwanamazoezi hufikiria mazoezi sharti ufanyie kwenye sehemu maalum ya mazoezi, la hasha mazoezi waweza fanyia hata ukiwa nyumbani, na  pia uwe unafanya kila siku na marudio mengi yasiyopungua mia sita kwa hesabu ya ishirini.

Yafuatayo ni baadhi ya mazoezi ya tumbo.


                               Namna ya kuanza zoezi la tumbo na kumalizia hapo juu


             Hapa unaaza mikono ikiwa nyuma ya kichwa ukinyanyuka unagusa
             magoti na kurudia hivyo mara kumi.


Zoezi hili ukiwa unaanza nakumaliza kama picha zinavyoonyeshanakaa mkao
 kama unapiga push up lakini unakunja mikono mmoja baada ya mwingine.

Hapa unakunja  mikono yako yote na unanyanyuka sehemu ya katina kukaa hivyo kwa muda wa sekunde 30 na urudie tena.










Saturday, September 5, 2015

MAMBO MUHIMU AMBAYO MJENGA MISULI YAANI BODY BUILDER ANATAKIWA KUFANYA NA CHAKULA ANACHOTAKIWA KULA.

Kama nilipozungumzia hapo awali kwa wale wapenzi wa kujenga misuli na kuonekana ana misuli mikubwa zaidi.Jambo la muhimu ni kupata miilo ambayo sio chini ya mara tano, hii ikiwa ni pamoja na kupata aina ya chakula cha protini ya kutosha, ambacho husaidia kukuza misuli kwa haraka na uhakika.

Kadhalika kupata aina ya chakula cha wanga ili kuupa mwili nguvu ya kuweza kunyanyua uzuto mkubwa kwa ajili ya kujenga misuli .Pia kupata muda wa kutosha kupumzika kwa ajili ya kuwezesha mwili kukuza misuli kwa matokeo ya mazoezi ya siku ile.

Hakikisha wakati wote tumbo lako lina chakula nikimaanisha kutokuwa na njaa kipindi chote.

Maji ni muhimu katika maisha ya mjenga misuli na pia mtu yeyote yule anayefanya mazoezi/

Monday, August 31, 2015

MASHINDANO YA WATUNISHA MISULI (BODY BUILDER) THE MOST MUSCULER MAN 2015


Mashindano yliyofana sana ambayo yalikuwa na washiriki kutoka Tanzania Bara na Visiwani  Zanzibar.

Hii ikiwa ni mara ya pili kufanyika  Dar es salaam na mwasisi Mohamed Ally ambaye ni mkurugenzi wa Tanzaned  Fitness iliyoko Gymkhana.

                     

                            Mkuu wa stegi Omar swai akiwa na Mr.India 
                            ambaye alialikwa kama mgeni katika kutunisha


Wanamisuli wakiwa katika mshindano ya kuonyesha
misuli ya tumbo kama picha inavyoonyesha




 

 
                         
 
 
 
 

 
                                Wshiriki  wakiwa wanasubiri kuingia katika gwee yao



 Mukurugenzi wa Tanzaned akiwa na mkuu wa wilaya ya
 Kinondoni wakimkabidhi zawadi ya cheki ya sh. 1500,000 
mshindi Omary aliyetokea mkoa wa Mbeya

 
 
 

Sunday, August 23, 2015

MWANA MAZOEZI ANATAKIWA MARA NGAPI KWA WIKI KUFANYA MAZOEZI KWA AFYA YAKO.

Mara nyingi katika suala la kufanya mazoezi kwa wana mazoezi  huwa na sintojua, mara ngapi kwa wiki unatakiwa kufanya mazoezi  ni wakati gani unatakiwa kuupumzisha mwili kwa ajili ya kujenga seli ambazo zimekufa katika mwili wa mwana mzoezi.

Mwana mazoezi anatakiwa kufanya mazoezi mara tano kwa wiki au mara tatu kama huwezi kufanya kwa siku tano. Nikisema hivyo nina maana mwili unahitaji kupumzishwa kutosha,ikiwa na kuhakikisha unalala sio chini ya masaa nane.

Pamoja na yote hayo kunywa maji ya kutosha kila siku ikiwa sio chini ya lita mbili,ni muhimu sana haswa kwa yule anayefanya mazoezi kila siku sababu mwili wa binaadam ni pasenti 60 ya maji.

Tuesday, August 11, 2015

WANAMAZOEZI WA AEROBICS UDSM WAKIWA NA KASI YA KUFANYA MZOEZI KWA AFYA ZAO


Mazoezi ni jambo la muhimu sana katika maisha ya kila siku.

 Ikiwa unataka kuishi kwa raha fanya mazoezi na pia yanarefusha umri wako.

                                                          Mazoezi ya Hi/Lo Aerobics 
                             

                                     


                               Wadau wa Aerobics wakifanya mazoezi hayo kwa umakini

                                H/ Lo Aerobics

Thursday, August 6, 2015

NI NAMNA GANI UNAWEZA KUPUNGUZA UZITO ULOKITHIRI

Watu wengi huona ugumu wa kupunguza uzito wa mwili wao lakini wengi wao hawajui madhara ya kuwa na uzito ulokithiri. Hii husababisha kuwa na tatizo la presha na kisukari.

Inatokea mpaka daktari akushauri kupunguza uzito, hapo ndipo anapoanza kuhangaika kuupunguza uzito ambao umemzidi na kusababisha madhara mwilini mwake.

Kuna njia muafaka wa kukufanya usiwe unaongezeka uzito mara kwa mara na njia yenyewe ni kubadilisha tabia ya kula hovyo na kuendekeza kusikia njaa na muda wa kupata maakuli ni bado.

Jaribu kula kwa wakati mmoja kama uliamua kula chakula cha mchana saa saba muda huo usipitilize ikiwa ni pamoja na kupunguza kiwango cha chakula unachokula kila siku.Hii itakusaidia kupunguza uzito ulokithiri,bila kusahau kufanya mazoezi ambayo yatakufanya kutoa jasho japo kwa muda wa dakika thelathini, kama una tabia ya kupenda kula kila wakati basi uwe unapata matunda pindi unapojisikia hivyo.

Usisahau wakati wa usiku pata chakula chepesi na uwe unakunywa maji kwa wingi japo lita mbili kwa siku, utakuwa na afya nzuri na uzito wako ulokithiri utapungua na hakikisha unalala muda wa saa nane wakati wa usiku.

Monday, July 13, 2015

NAMNA YA MIPANGILIO YA KULA VYAKULA KWA AJILI YA KUJENGA MWILI NA KUJIKINGA NA MARADHI

AINA ZA VYAKULA NA WAKATI  MUAFAKA WA KULA

1.Aina ya vyakula vya wanga.

Chakula hiki ni kwa ajili ya kuupa mwili nguvu na mara nyingi hutumika wakati wa mchana kwa sababu unafanya kazi iwe ni ya ofisini au shambani, aina yenyewe ni kama vile ugali wa dona,wali,ugali wa mtama na ngano.

2.Aina ya vyakula vya protini.

Chakula hiki kinasaidia katika kujenga misuli ya mwili ni muhimu sana haswa kutumika kwa wale wanaofanya mazoezi ya kujenga misuli,pia ni vizuri kuliwa  wakati wa asubuhi na jioni na aina yenyewe ni nyama ya kuku, mayai ya kuku, maharage na samaki.

Bila kusahau aina ya mbogamboga na matunda yawemo japo kwenye mlo mmoja.


Sunday, June 21, 2015

MADHARA NA HASARA YA KUWA NA KITAMBI KWA AFYA YAKO


Wako baadhi ya watu ambao wanaona fahari ya kuwa na kitambi tena hujisifu na kusema kama huna kitambi hutopata heshima na kuonekana mchovu yaani huna pesa.

Mimi sikubaliani nao abani  nawaonea huruma kwani tayari wameshakuwa ni wagonjwa japo wao hujiona ni afya.

Kuwa na kitambi ni maradhi ambayo unatembea nayo lakini baada ya siku unakuja kugundua kumbe ulikuwa mgojwa, kwa sabababu kuwa na kitambi  ni mkusanyiko wa mafuta yaliyokithiri mwilini ambayo hutakiwi kuwa nayo.

Mwanadamu kwa kawaida akizidiwa na mafuta mwilini huwa anakuwa na uwezekano mkubwa wa kupata maradhi ya presha na tena isitoshe ni rahisi pia kupata ugonjwa wa kisukari.

Nawashauri wale wenye vitambi kuondoa mawazo potofu ya kuonekana na kitambi ni heshima, fanya mazoezi kwa ajili ya afya yako, punguza uzito ulokithiri hapo ndipo utafanya mambo yako ya kila siku na kujisikia mwepesi na kuonekana na mvuto hata ukivaa nguo zako. 

Monday, June 8, 2015

MAZOEZI YA AEROBICS YANAVYOSAIDIA KUPUNGUZA UZITO KATIKA GYM YA UDSM



MAZOEZI YA AEROBICS YANAVYOWANUFAISHA WADAU WA MAZOEZI KATIKA GYM YA UNIVERSITY MLIMANI KATIKA PICHA MBALI MBALI .








Sunday, May 17, 2015

MWANA MAZOEZI MKONGWE FRANCIS MSANGI AMBAYE AMEFANIKIWA SANA KATIKA KUFANYA MAZOEZI.


Mara  nyingi ukizungumzia mazoezi lazima umkute mwana mazoezi mkongwe yupo na sio kwa mazoezi ya ndani  yani gym, hata kushiriki katika mshindano ya kukimbia marathon.

Huyu ni Mwanasheria anayejitegemea  mwana mazoezi Farancis  Msangi na pia ni mpenzi wa  gym ya UDSM.

Akizungumzia mikasa iliyomkuta  alikuwa anasumbuliwa na kisukari lakini tangu aanze mazoezi miaka miwili iliyopita amepona kabisa yuko poa.


                                    Mwana mazoezi  Francis Msangi akifanya moja ya 

                                      mzoezi ya tumbo


   
           Franscis akiwa anafanya zoezi kwenye mashine ya 

cross training.

Friday, April 24, 2015

AINA YA VYAKULA UNAVYOTAKIWA KULA NA NYAKATI ILI KUEPUKA ONGEZEKO LA UZITO WA MWILI WAKO



Kwa  bahati nzuri hapa kwetu  Tanzania tumejaaliwa kuwa na vyakula vya kila aina na uwezo wakuvipata kirahisi kwa namna moja au nyingine tunayo.

Mara nyingi  huwa naulizwa ni wakati gani muafaka wa kula vyakula vya wanga na wakati upi kula vyakula aina  ya protini.

*Mwili wa binaadamu unahitaji aina ya vyakula vya wanga kwa nyakati za mchana kwa sababu ya kukupa nguvu kwa shughuli zako za mchana maana katika utendaji kazi huwa matumizi ya nguvu hutumika sana.(kama vile ugali wa muhogo,wali,chapati,makaroni nk.)

Chakula aina ya protini kwa matumizi ya usiku ni muhimu hii ikiwa na maana  vyakula vya aina ya protini sio rahisi kugeuka kuwa mafuta, hii nikimaanisha huenda kiurahisi kwenye mwili bila ya kurundikana kutokana na matumizi yake ni kila wakati mwilini bila ya kutumia nguvu.( kama vile mboga za majani, samaki,kuku,maharage meupe na matunda ya msimu.)

Kumbuka kuepuka kuongezeka uzito jaribu kula vyakula laini nyakati za usiku.(dinner)


Friday, March 20, 2015

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI HATA UKIWA NYUMBANI KWAKO BILA YA KWENDA KITUO CHA MZOEZI( GYM)



Watu wengi wanafikiri kuwa kufanya mazoezi  ni lazima uende kituo cha kufanyia  mazoezi (gym)  au uwanjani, la hasha hakuna ulazima huo bali  unaweza pia kufanyia hata ukiwa ndani mwako ili mradi kuwe na nafasi ya mita moja pande zote nne.

NAMNA YA KUANZA NA KUMALIZIA ZOEZI
Unasimama huku miguu yako imepanuka na kuweka mziki wa aina yoyote ile uipendayo wewe na kuanza kucheza muziki huo kwa muda wa dakika 5 halafu unasimama.
Utapumzika kwa sekunde 30 na kurudia hivyo aidha kwa kuruka ruka ili mradi unaongozwa na muziki wako uupendao.

Utaendelea kufanya hivyo hadi umalizapo aina 5 ya muziki utakuwa umeatokwa na jasho sio la kawida hii itakusaidia wewe kupunguza zile kaloriz ambazo zimezidi mwilini mwako.
Baada ya hapo ukae hadi jasho likauke ndipo uendelee kuoga.
Zoezi hili huchukua muda wa dakika25 tu.

Friday, February 27, 2015

AINA YA VYAKULA UNAVYOTAKIWA KULA ILI KUEPUKA MARADHI YA KISUKARI


Pamoja na kufanya mazoezi ili kuepukana na maradhi ya kisukari, pia inahitajika kujua aina gani ya vyakula unavyotakiwa kula.
Hii imesisizwa sana  vyakula ambavyo havikobolewi ikiwemo dona badala ya sembe na aina nyingine ni kama ulezi, mtama na matunda.
Halikadhalika kuepukana na vinywaji ambavyo huwekwa sukari nyingi kama vile soda,pombe na juisi kwa sababu vinywaji hivi huenda moja kwa moja kwenye utumbo mwembamba na kulazimisha kongosho linalozalisha kemikali ya insulin kufanya kazi kwa kiwango cha juu isivyo kawaida.
Hivyo basi vyakula ambavyo havikobolewi huchukua muda kusagika na kwenda kwenye utumbo mwembamba hivyo husagwaswagwa vyema na kuenda kwenye matumizi ya mwili.
Halikadhalika yale makapi ambayo hutokana na hivyo vyakula husaidia kuzuia kupata kansa ya utumbo.


                        Namna moja ya zoezi la push up ili kuepuka maradhi ya kisukari


                      Step Aerobics kwa ajili ya kuweka mwili afya na kuepuka maradhi.

Monday, February 16, 2015

UMUHIMU WA KUFANYA MAZOEZI ILI KUEPUKA MARADHI YA KISUKARI


Mara nyingi sisi binaadamu hatufanyi kitu bali kwa manufaa fulani tena pale unapozidiwa na kushuriwa na daktari ndipo tunazinduka.
Mazoezi ni jambo la muhimu sana kwa binaadamu yeyote yule kufanya ili kuepukana na maradhi ambayo yanasumbua binaadamu.
Leo nizungumzie maradhi ya kisukari kwa ufupi ni namna gani yanakupata na jinsi ya kuepuka.
Kuna umuhimu wa kila mtu kufanya mazoezi yasiyopungua muda wa dakika 30 hadi saa moja kila siku katika maisha  yake ili kuepuka maradhi haya ya kisukari, hii inasaidia mwili wote ikiwa pamoja na misuli kufanya mazoezi  na kutokwa na jasho ambayo husaidia hutumia kiasi cha sukari kinachozalishwa mwilini.Hii ni kwa sababu mwili wa binadamu huzalisha sukari kila siku na inatakiwa ile sukari itumike ipasavyo bila kuwa na kusanyiko mwingi wa sukari mwilini.



                                         Mzoezi ya rowwing namna unavyoanza

                                Mazoezi ya rowwinng unapomalizia hufanya kwa dk 25 tu.

Monday, January 26, 2015

MAZOEZI YA DOUBLE STEP NEW VISION


MAZOEZI YA  DOUBLE STEP NEW VISION JINSI PICHA ZIKIONYESHA YAFANA SANA UDSM GYM






                              Katika hizo picha hapo juu inaonekana kila mtu amegeuka upande wake
                                lakini  ni aina moja ya ufuatilio wa zoezi hilo

Thursday, January 8, 2015

MWAKA MPYA NA ARI MPYA YA WANAMAZOEZI


Mazoezi sio lazima uwe unacheza mpira wa miguu au kukimbia tu kuna aina nyingi za mazoezi ambayo ukiyafanya yatakusaidia na kukuweka na afya kila wakati.
Hii ikiwa ni pamoja na mazoezi utakayofanya ukiwa nyumbani au hata ukiwa maeneo ya gym yakiongozwa na mwalimu mwenye taaluma hii.
Ni muhimu kuwa na mwalimu mwenye taaluma hii kuwepo ili kuepuka maumivu yasiyoisha baada ya mazoezi.
                                                         







                                                Hapo katika picha ya juu ni zoezi la
                                                tumbo inavyoanza na kumalizia.


                                       Mazoezi ambayo husaidia kunyoosha viungo
                                      baada ya mazoezi mazito ili kuondoa uchovu