Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Wednesday, September 28, 2011

UMUHIMU WA MATAYARISHO KABLA YA KUANZA MAZOEZI (WARM UP)

Wadau wa mazoezi ya viungo leo ngoja niwakumbushe umuhimu wa kufanya mazoezi ya kupasha mwili moto(warm up) kabla ya kuanza zoezi lolote.

Umuhimu wa kufanya hilo zoezi la kupasha mwili moto(WARM UP) ni kuutayarisha mwili kwa mazoezi. Pia husaidia kuongeza usambazaji wa damu katika viungo pamoja na misuli ya mwili pamoja na kuupa mwii joto kwa matayarisho ya mazoezi utakayofanya ambayo husaidia kulainisha viungo vyako vya mwili, hata hivyo husaidia kulainisha mishipa inayopeleka damu kwenye moyo na kusaidia kulinda misuli isipate madhara pamoja na mifupa.

Vilevile kupasha mwili moto(warm up) husaidia kuongezeka upatikainaji wa hewa ya oksijen kwenye misuli na mishipa ya fahamu kwa binaadamu anayefanya mazoezi.

Hivyo mdaua wa mazoezi huo ndio umuhimu wa kupasha mwili moto( warm up) kabla ya kufanya mazoezi.

Friday, September 23, 2011

MAZOEZI YA MGONGO NA UTI WA MGONGO

MAZOEZI YA MGONGO JINSI YANAVYOANZA NA KUMAZIA















Unaanza mazoezi kama picha inavyoonyesha juu















Unamalizia kama picha inavyoonyesha hapo
kwa kurudia 10x10





















Hapa chini ni mazoezi ya uti wa mgongo

Tuesday, September 6, 2011

MAZOEZI AMBAYO MTU YEYOTE ANAWEZA FANYA AKIWA NYUMBANI

Baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhan nadhani kila mtu sasa anayofursa ya kufanya mazoezi ya viungo bila ya kuwa na kiwazo labda awe anaumwa. Lakini ukiwa mzima jaribu kufanya mazoezi kama hayo yanasaidia sana kwa kuzingatia maelekezo yake.

















Mazoezi unayoyaona kwenye picha hapo juu ni mazoezi ya sehemu ya mgongo unafanya hivyo na kulala huku mikono yako ikiwa umekita pembeni mwa kifua na kuhakikisha mapaja yanabaki chini kinacho inuka ni sehemu ya juu kama picha inavyoonyesha. Unafanya mara kumi unapumzika halafu unarudia tena kwa mara tatu yaani 10x3 jumla iwe ni mara 30


















Hapa ni mazoezi ya sehemu ya pembeni mwa mbavu(oblique) mazoezi haya yanasaidia kutoa manyama uzembe yaliyo pembeni mwa kiuno na kwenye maeneo ya mbavu kwa kutumia mkono mmoja kupita juu ya kichwa chako kama picha inavyoonyesha hapo juu unafanya 10x3 kila upande.















Mazoezi haya ni saw na yaliyotangulia lakini unatumia mikono yote kama picha inavyoonyesha.