Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Saturday, April 17, 2010

UBAYA WA KUWA NA KITAMBI

Katika maisha ya kawaida kuna watu wengi hupenda kuwa na kitambi kwa sababu eti, ukiwa na kitambi wewe ni tajiri una pesa na wengine hudhubutu kusema ni heshima ukiwa na kitambi.

Hapana hizo ni fikra potofu kabisa,kitambi siyo afya bali ni ugonjwa. Maana ukishakuwa na kitambi uwezo wa mambo fulani hupungua hata ukitembea hatua chache huwa unahema sana kama umekimbia.

Maana kwenye hicho kitambi kilichopo ndani yake ni mafuta matupu, hivyo hata moyo wako unakuwa umezingirwa na mafuta kiasi cha kutofanya kazi yake ya msukumo wa damu kwenye mwili ipasavyo kwa kuchelewa kepeleka damu kwanye mwili inabidi moyo ufanye kazi yake kwa ugumu ndipo unajikuta una tatizo la presha kupanda, ukienda kumuona daitari hukushauri kupunguza uzito au kutokula vitu vya mafuta.

Dawa yake ni kufanya mazoezi kila siku hii, itakusaidia kuondoa mafuta ambayo yamezingira moyo wako usifanye kazi yake inavyopaswa. Fanya mazoezi epuka maradhi kama haya.

No comments: