Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Thursday, April 29, 2010

NAMNA YA KUFANYA YA MPANGILIO WA KULA CHAKULA KWA WALE AMBAO WANATAKA KUPUNGUZA UZITO.

Kwa wale ambao ni mara yao ya kwanza kabisa kufanya hili zoezi la kupunguza uzito, wataona ni vigumu lakini ukizingatia haya maelezo basi wewe utafanikiwa. Jaribu kuwa unajiamini kwanza kwa kuamua kupunguza uzito uliokithiri, jaribu sana kupangilia mda wako wa kula ikiwa unakula chakula cha mchana saa 7 iwe ni kawaida yako kula mda ulopangia.

Mlo wa siku ni chai ya asubuhi ua kifungua kinywa nikiwa na maana kama upate chai ya kutosha wakati wa asubuhi.
Kwa sababu unapopata chai ya kutosha ndivo hutotamani kula hovyo hovyo bila ya mpangilio mpaka ule muda wako wa kupata chakula cha mchana.

Namna ya kujipangia miilo yako:
-Jaribu kupunguza kiasi cha chakula unachokula kila siku (ikiwa unakula sahani ilojaa unakula nusu yake).
-Punguza mafuta kwenye chakula unachotumia.
-Punguza sukari katika chai, au vitu vitamu kama keki, soda,na choklet.
-Punguza pia chumvi kwenye mlo wako yaani ile chumvi ya kuongeza mezani.
-Jaribu kuchukua muda pindi unapokula chakula nikiwa na maana utafune chakula hadi kilainike,hii inasaidia kurahisisha usagaji chakula kwa urahisi tumboni na kwa muda unaotakiwa kusambaza kwenye mwili kupitia mishipa ya damu na kupeleka mwilini.
-Mlo wa usiku jaribu kupata chakula laini na ule mapema kama saa 3 kabla ya kulala.
- Mazoezi ni muhimu wakati unafanya diety.

No comments: