Powered By Blogger

Kuna umuhimu wa kufanya mazoezi?

Tuesday, February 4, 2014

MWANA MAZOEZI ALIYEPATA FAIDA KUBWA KUFANYA MAZOEZI YA AEROBICS




Mwana mazoezi Charles Mapima amefaidika sana katika kufanya mazoezi ya aerobics ambayo yamemsaidia kiasi kikubwa katika maisha yake ya kila siku.
Akitoa ushuhuda kwangu mie kuwa alikuwa akisumbuliwa na presha pamoja na maimivu makali ambayo alikuwa anapata wakati wa kutembea na hata kukaa kwenye nyonga.
Lakini alipofanya mazoezi ya aerobics takriban miezi sita iliyopita yale maumivu ya nyonga yamekwisha bila ya kutumia dawa yoyote ile.Hata lile tatizo la presha limekwisha kabisa alipokwenda kumuona daktari wake kupima,amekuwa ni mtu wa furaha na afya bora kutokana na umri wake mkubwa.


            Mwana mazoezi mzee Charles Mapima akiwa katika mazoezi ya step aerobics
                     akiwa kalowa jasho tishet yake hii husaidia kukata kalori zilizozidi mwilini.

No comments: